Jeneza la Milly wa Doc la KSh 100k na Bajeti ya Mazishi Yawashangaza Wakenya: "Chakula ni KSh 300k"

Jeneza la Milly wa Doc la KSh 100k na Bajeti ya Mazishi Yawashangaza Wakenya: "Chakula ni KSh 300k"

  • Familia ya TikToker maarufu Milly wa Doc inapanga kumzika kwa hafla ya kifahari na imeomba msaada wa michango kutoka kwa Wakenya
  • Kwa mujibu wa mwenyekiti wa kamati ya mazishi, wanahitaji pesa kwa ajili ya mavazi ya mazishi ya familia, usafiri, ulinzi, pamoja na gharama nyinginezo
  • Wakenya wameonyesha maoni yao kuhusu bajeti hiyo kubwa, na kuwashauri jamaa wa Milly kuhusu jinsi ya kupunguza baadhi ya gharama

Familia ya Milly wa Doc, ambaye alikuwa mchangamfu na mwenye mvuto mitandaoni, inawaomba Wakenya kuwasaidia kuchangisha KSh 2.5 milioni ili kugharamia mazishi na mahitaji mengine.

Jeneza la Milly wa Doc la KSh 100k na Bajeti ya Mazishi Yawashangaza Wakenya: "Chakula ni KSh 300k"
Milly wa Doc alifariki mwezi mmoja baada ya kutangaza ameolewa na Odeke. Picha: Milly wa Doc.
Chanzo: TikTok

Sababu ya kifo cha Milly wa Doc

Milly wa Doc, ambaye jina lake halisi ni Milka Nyatuga, alifariki dunia mnamo Juni 3 katika Hospitali ya Rufaa na Mafunzo ya Kaunti ya Nakuru alipokuwa akipokea matibabu.

Daktari James Waweru, akizungumza na NTV, alieleza kuwa Milly alifikishwa hospitalini akiwa anavuja damu sana, baada ya kurejelewa kutoka hospitali binafsi.

Alikuwa mjamzito kwa takribani miezi sita. Alitibiwa, akapewa damu, na kisha kufikishwa kwenye chumba cha upasuaji ambapo walitoa kijusi.

Baada ya upasuaji uliofanikiwa, madaktari waligundua kuwa figo zake hazikuwa zikifanya kazi vizuri.

Alianza kupokea matibabu, lakini akafariki kutokana na matatizo ya ujauzito. Ilibainika pia kuwa Milly alikuwa amelazwa hospitalini hapo hapo mwezi Aprili kwa matatizo yale yale ya ujauzito.

Gharama za mazishi ya Milly wa Doc

Katika mkutano wa kifamilia uliorushwa moja kwa moja kupitia TikTok, mwenyekiti wa mazishi alitangaza bajeti ya takriban KSh 1.4 milioni.

Hapa chini ni baadhi ya vipengele vya bajeti hiyo:

Jeneza: KSh 100,000

Hifadhi ya maiti: KSh 50,000

Gari la kusafirisha mwili: KSh 50,000

Mavazi ya familia: KSh 200,000

Gauni la marehemu: KSh 50,000

Usafiri wa familia: KSh 30,000

Maji yaliyochapishwa picha ya marehemu: KSh 20,000

Kuchapisha wasifu: KSh 30,000

Maua: KSh 20,000

Mahema mawili na gazeebo: KSh 20,000

Viti: KSh 20,000

Polisi wawili kwa usalama: KSh 5,000

Walinzi binafsi 10: KSh 10,000

Maji kwa harambee: KSh 10,000

Chakula na upishi: KSh 300,000

Bili ya hospitali: KSh 10,000

Burudani: KSh 20,000

MC: KSh 5,000

Mchungaji: KSh 5,000

Mpiga picha: KSh 45,000

Picha ya marehemu: KSh 5,000

Kodi ya nyumba: KSh 165,000

Ada ya shule ya Sheila: KSh 25,000

Jumla: KSh 1,395,000

Maoni ya wanamtandao kuhusu bajeti ya mazishi

Wanamtandao walionyesha hisia mseto, wengi wakikosoa bajeti hiyo kwa kusema ni ya kupindukia:

Quinta-official: "Niko hapa kukumbusha hii familia mpige budget ya pesa mkonayo."

Marydee: "Kwani watoto wawili wanavaa nguo ya 200k, mko na vituko nyinyi."

ABBY: "Jeneza 100,000?"

Fridah: "Hiyo 200k lipa malimbikizo ya karo na nyumba."

Adrian's mum: "Wanataka branded water na picha za marehemu/security/100k coffin yet kuna arrears?"

Mirry: "Wazike alafu warudi kwao wakule hiyo 300k ipewe Brayo for life setup gosh."

It’s me: "Watu wachangie watoto baada ya mazishi, hiyo pesa wanaitisha watoe wao."

Maelezo zaidi kuhusu maisha na kifo cha Milly wa Doc

Mpenzi wake wa zamani, Jim Bonnie, aliandika ujumbe wa kuhuzunisha kumkumbuka.

Ujumbe wake wa mwisho kwa mwanawe siku ya kuzaliwa ulimgusa kila mmoja.

Video ya zamani ikionyesha akitabiri kifo chake ilisambaa baada ya kufariki.

Alitamani kuchomwa (cremation) baada ya kifo chake.

Alifunga ndoa na Odeke mwezi Aprili, na waliwaonyesha hadharani mapenzi yao bila woga.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsApp: 0732482690.

Chanzo: TUKO.co.ke

Authors:
Shillah Mwadosho avatar

Shillah Mwadosho (Swahili editor) Shillah Mwadosho ni mwandishi wa habari wa TUKO.co.ke katika kitengo cha Kiswahili tangu 2019. Ana tajriba ya takriban miaka minne katika fani ya uandishi wa habari kwenye redio, televisheni na gazetini. Alipata ujuzi wa uanahabari katika taasisi ya Alphax mjini Eldoret. Yeye hujituliza kwa kusikiza muziki na kufurahia densi baada ya kazi. Email: [email protected]

OSZAR »