Jeneza la Milly wa Doc la KSh 100k na Bajeti ya Mazishi Yawashangaza Wakenya: "Chakula ni KSh 300k"
- Familia ya TikToker maarufu Milly wa Doc inapanga kumzika kwa hafla ya kifahari na imeomba msaada wa michango kutoka kwa Wakenya
- Kwa mujibu wa mwenyekiti wa kamati ya mazishi, wanahitaji pesa kwa ajili ya mavazi ya mazishi ya familia, usafiri, ulinzi, pamoja na gharama nyinginezo
- Wakenya wameonyesha maoni yao kuhusu bajeti hiyo kubwa, na kuwashauri jamaa wa Milly kuhusu jinsi ya kupunguza baadhi ya gharama
PAY ATTENTION: Flexible Payment Plans Available! Invest in Yourself & See the Return with Our Affordable Copywriting Course!
Familia ya Milly wa Doc, ambaye alikuwa mchangamfu na mwenye mvuto mitandaoni, inawaomba Wakenya kuwasaidia kuchangisha KSh 2.5 milioni ili kugharamia mazishi na mahitaji mengine.

Chanzo: TikTok
Sababu ya kifo cha Milly wa Doc
Milly wa Doc, ambaye jina lake halisi ni Milka Nyatuga, alifariki dunia mnamo Juni 3 katika Hospitali ya Rufaa na Mafunzo ya Kaunti ya Nakuru alipokuwa akipokea matibabu.
Daktari James Waweru, akizungumza na NTV, alieleza kuwa Milly alifikishwa hospitalini akiwa anavuja damu sana, baada ya kurejelewa kutoka hospitali binafsi.
Alikuwa mjamzito kwa takribani miezi sita. Alitibiwa, akapewa damu, na kisha kufikishwa kwenye chumba cha upasuaji ambapo walitoa kijusi.
Baada ya upasuaji uliofanikiwa, madaktari waligundua kuwa figo zake hazikuwa zikifanya kazi vizuri.
Alianza kupokea matibabu, lakini akafariki kutokana na matatizo ya ujauzito. Ilibainika pia kuwa Milly alikuwa amelazwa hospitalini hapo hapo mwezi Aprili kwa matatizo yale yale ya ujauzito.
Gharama za mazishi ya Milly wa Doc
Katika mkutano wa kifamilia uliorushwa moja kwa moja kupitia TikTok, mwenyekiti wa mazishi alitangaza bajeti ya takriban KSh 1.4 milioni.
Hapa chini ni baadhi ya vipengele vya bajeti hiyo:
Jeneza: KSh 100,000
Hifadhi ya maiti: KSh 50,000
Gari la kusafirisha mwili: KSh 50,000
Mavazi ya familia: KSh 200,000
Gauni la marehemu: KSh 50,000
Usafiri wa familia: KSh 30,000
Maji yaliyochapishwa picha ya marehemu: KSh 20,000
Kuchapisha wasifu: KSh 30,000
Maua: KSh 20,000
Mahema mawili na gazeebo: KSh 20,000
Viti: KSh 20,000
Polisi wawili kwa usalama: KSh 5,000
Walinzi binafsi 10: KSh 10,000
Maji kwa harambee: KSh 10,000
Chakula na upishi: KSh 300,000
Bili ya hospitali: KSh 10,000
Burudani: KSh 20,000
MC: KSh 5,000
Mchungaji: KSh 5,000
Mpiga picha: KSh 45,000
Picha ya marehemu: KSh 5,000
Kodi ya nyumba: KSh 165,000
Ada ya shule ya Sheila: KSh 25,000
Jumla: KSh 1,395,000
Maoni ya wanamtandao kuhusu bajeti ya mazishi
Wanamtandao walionyesha hisia mseto, wengi wakikosoa bajeti hiyo kwa kusema ni ya kupindukia:
Quinta-official: "Niko hapa kukumbusha hii familia mpige budget ya pesa mkonayo."
Marydee: "Kwani watoto wawili wanavaa nguo ya 200k, mko na vituko nyinyi."
ABBY: "Jeneza 100,000?"
Fridah: "Hiyo 200k lipa malimbikizo ya karo na nyumba."
Adrian's mum: "Wanataka branded water na picha za marehemu/security/100k coffin yet kuna arrears?"
Mirry: "Wazike alafu warudi kwao wakule hiyo 300k ipewe Brayo for life setup gosh."
It’s me: "Watu wachangie watoto baada ya mazishi, hiyo pesa wanaitisha watoe wao."
Maelezo zaidi kuhusu maisha na kifo cha Milly wa Doc
Mpenzi wake wa zamani, Jim Bonnie, aliandika ujumbe wa kuhuzunisha kumkumbuka.
Ujumbe wake wa mwisho kwa mwanawe siku ya kuzaliwa ulimgusa kila mmoja.
Video ya zamani ikionyesha akitabiri kifo chake ilisambaa baada ya kufariki.
Alitamani kuchomwa (cremation) baada ya kifo chake.
Alifunga ndoa na Odeke mwezi Aprili, na waliwaonyesha hadharani mapenzi yao bila woga.
Read ENGLISH VERSION
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsApp: 0732482690.
Chanzo: TUKO.co.ke