Mama Aliyekimbizwa Hospitalini na Kujifungua Mapacha 3 Azuiwa Kuondoka Hadi Alipe KSh 140k

Mama Aliyekimbizwa Hospitalini na Kujifungua Mapacha 3 Azuiwa Kuondoka Hadi Alipe KSh 140k

  • Esther Wanjiru Wanjira amekwama katika hospitali ya kibinafsi jijini Nairobi, wiki moja baada ya kujifungua watoto watatu
  • Mama huyo mwenye umri wa miaka 38 hawezi kuondoka katika kituo hicho kutokana na bili inayozidi kuwa kubwa kila kukicha ambayo imefikia KSh 140,000
  • Anaomba msaada wa fedha ili kupata fedha hizo ili aweze kuondoka na kuhamishiwa katika Hospitali ya Kujifungulia ya Pumwani, ambako gharama ya huduma ni ndogo

Esther Wanjiru Wanjira anaomba msaada baada ya kuzuiliwa katika hospitali ya kibinafsi jijini Nairobi, ambapo alijifungua watoto watatu kwa dharura wiki jana.

Mama Aliyekimbizwa Hospitalini na Kujifungua Mapacha 3 Azuiwa Kuondoka Hadi Alipe KSh 140k
Wanjiru anatarajia kuhamishiwa katika hospitali ya umma ambapo gharama zake zinaweza kudhibitiwa. Picha: Mercy Wairimu Okwero.
Chanzo: UGC

Mama huyo mwenye umri wa miaka 38, ambaye alikuwa akijifungua kwa mara ya kwanza, alikimbizwa katika kituo hicho cha afya mnamo Mei 6, 2025, saa 3 usiku na kujifungua siku hiyo hiyo.

Bili ya hospitali anayodaiwa Wanjiru ni kiasi gani?

Sasa, siku saba baadaye, mama huyo wa watoto watatu hawezi kuondoka hospitalini kutokana na bili kubwa inayozidi kila kukicha ambayo imefikia KSh 140,000.

Kufikia sasa, familia hiyo imefaulu kuchangisha KSh 80,000 lakini inasema hospitali imekataa kumfukuza hadi kiasi kamili kilipwe.

Dadake Wanjiru, Mercy Wairimu Okwero, aliambia TUKO.co.ke kuwa uamuzi wa kutumia hospitali hiyo ya kibinafsi haukuwa wa lazima.

"Tulifika tu kwenye kituo cha kibinafsi kwa sababu ilikuwa dharura, lakini hatuwezi kuendelea kumuweka hapa," dada Wairimu alisema.

Jinsi ya kuchangia bili ya hospitali ya Wanjiru

Mercy na nduguye wanatafuta mama huyo mpya kuhamishiwa katika Hospitali ya Kujifungulia ya Pumwani, kituo cha umma ambapo gharama ya huduma ni ya chini sana.

Hata hivyo, hospitali ya sasa inasisitiza kwamba bili iliyosalia lazima itatuliwe kabla ya uhamisho wowote kuruhusiwa.

Kinachowatia wasiwasi ni kwamba bili inaendelea kulimbikizwa kila siku ya ziada anayotumia kwenye kituo hicho.

Familia hiyo sasa inawaomba watu wenye mapenzi mema usaidizi wa kuwasaidia kulipa salio lililosalia ili Wanjiru na watoto wake wachanga waweze kupata huduma ya bei nafuu zaidi.

Michango inaweza kutolewa kupitia Paybill 247247, nambari ya Akaunti 0722579576.

Mama Aliyekimbizwa Hospitalini na Kujifungua Mapacha 3 Azuiwa Kuondoka Hadi Alipe KSh 140k
Wanjiru akipiga picha na watoto wake wachanga, ambao bado wako NICU. Picha: Mercy Wairimu Okwero.
Chanzo: UGC

Mama kutoka Diani, mwanawe mchanga wazuiwa hospitalini

Kwingineko, Priscilla Kyove Kyumwa hivi karibuni alifanyiwa upasuaji wa dharura katika Hospitali ya Diani na kujifungua mtoto wa kike.

Alitokwa na damu kwa ndani ambayo ilihitaji upasuaji wa pili, wakati mtoto wake aliyezaliwa kabla ya wakati aliwekwa katika Chumba cha Uangalizi Maalumu wa Watoto wachanga (NICU).

Mama na mtoto wake wanaendelea vyema, lakini wamekwama hospitalini kwa bili inayosubiriwa ya KSh 1.5 milioni na wanatafuta usaidizi kutoka kwa Wakenya.

Simu ya dakika ya mwisho yaokoa mwanamke wa Nakuru aliyekwama hospitalini

Huko Nakuru, kilichoanza kama safari ya matumaini kuelekea uponyaji kiligeuka kuwa kungoja kwa muda mrefu na chungu kwa Wangeci Alice.

Hii ni baada ya upasuaji wake wa nyonga uliosubiriwa kwa muda mrefu kutofikiwa kutokana na kucheleweshwa mara kwa mara kwa idhini na Mamlaka ya Afya ya Jamii (SHA).

Akiwa amechanganyikiwa, alichapisha kwenye Facebook akionyesha kwamba alikuwa karibu kuacha matibabu yake.

Chapisho lake lilisambaa kwa kasi, na kusababisha uingiliaji kati wa haraka na simu ya dakika ya mwisho ambayo iliokoa siku, na kuandaa njia ya upasuaji wake.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsApp: 0732482690.

Chanzo: TUKO.co.ke

Authors:
Francis Silva avatar

Francis Silva (Swahili translator) Francis M Silva ni Mkuu wa Kitengo cha Kiswahili. Ana tajriba ya miaka mingi katika taaluma ya uwanahabari hasa tafsiri, uhariri - Radio, TV na Dijitali. Yeye ni zao la Taasisi ya Mawasiliano-Umma ya Kenya (KIMC). Wasiliana naye kupitia: [email protected]

OSZAR »