Mama Nandi Atafuta Usaidizi wa Kumpata Bintiye Aliyetoweka 2017: "Kitinda Mimba Wangu"
- Victoria Chepkosgei, ambaye alikuwa mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Kenyatta, alitoweka 2017 katika hali ya kutatanisha
- Mamake, Milka Rono, aliambia TUKO.co.ke kwamba alimtembelea mpenziwe huko Webuye na alitarajiwa kurejea nyumbani kujiandaa kwa shule, lakini hakuwahi kuonekana tena
- Siku alipotoweka, Victoria alimpigia simu mamake kutoka Eldoret kumwambia kuwa anarudi nyumbani, lakini simu yake ilizimwa saa chache baadaye
- Mwanamke huyo aliyevunjika moyo anatoa wito kwa umma na wanamtandao kutoa taarifa zozote zinazoweza kusaidia kumrudisha bintiye nyumbani
PAY ATTENTION: Flexible Payment Plans Available! Invest in Yourself & See the Return with Our Affordable Copywriting Course!
Familia moja katika kaunti ya Nandi inaomba usaidizi wa kumpata binti yao, Victoria Chepkosgei, aliyetoweka miaka minane iliyopita.

Chanzo: UGC
Mamake aliyekuwa amehuzunika, Milka Rono, aliambia TUKO.co.ke kwamba Victoria alikuwa mwanafunzi katika Chuo Kikuu cha Kenyatta alipotoweka.
Victoria Chepkosgei alionekana wapi mara ya mwisho?
Milka alisema bintiye ambaye ni kitinda mimba, alikuwa ameenda kumtembelea mpenziwe huko Webuye, kaunti ya Bungoma, kwa muda na alitakiwa kurejea nyumbani kujiandaa kwa shule, lakini hakuonekana tena.
"Haikuwa mara ya kwanza kumtembelea. Wakati mwingine shule zilipofungwa, alikuwa akimtembelea Webuye kabla ya kurudi nyumbani. Wakati huu hakufika nyumbani," alisema Milka.
Mama huyo aliyefadhaika alisema kwamba siku ambayo bintiye alitoweka, Victoria alimpigia simu na kumwambia kwamba alikuwa akielekea nyumbani na alikuwa amefika Eldoret, lakini saa chache baadaye simu yake ilizimwa.
"Mpenzi wake, Kevin Muyoma, alituambia kwamba Victoria alikuwa ameondoka, akisema alikuwa anakuja nyumbani na hajui aliko au kusikia kutoka kwake," aliongeza.
Milka alisema walitafuta kila mahali, ikiwa ni pamoja na kuripoti kutoweka kwake katika Chuo Kikuu cha Kenyatta, lakini waliambiwa kuwa wakati mwingine wanafunzi hutoweka tu.

Chanzo: UGC
Alibaini kuwa mumewe alikufa mnamo 2024, na alitamani Victoria angehudhuria mazishi, lakini juhudi zote za kumpata hazikufaulu.
"Wakati fulani mimi huhisi kuchoka kungoja. Ukurasa wake wa Facebook umebaki bila kufanya kazi tangu alipotoweka, na hajibu ujumbe wowote-hata marafiki zake wanapomtakia heri ya siku yake ya kuzaliwa. Angekuwa na umri wa miaka 27 sasa," alisema.
Alionyesha matumaini ya kumpata bintiye mzaliwa wa kwanza na kutoa wito kwa Wakenya ambao huenda walimwona kuripoti katika kituo cha polisi kilicho karibu nao au wawasiliane naye moja kwa moja kupitia nambari yake ya simu ya rununu 0723509391.
"Nimewaomba wajukuu zangu, ambao wako kwenye mitandao ya kijamii, wanisaidie kumtafuta mtandaoni. Ninahisi uchovu na huzuni lakini nina matumaini kwamba nitampata," alisema.
Mchungaji wa Kericho aliyetoweka hospitalini apatikana salama
Kwingineko, TUKO.co.ke iliripoti kuwa familia moja katika kijiji cha Kimasian, kaunti ya Kericho ilipumua baada ya kumpata mwana wao, Gideon Kipkoech.
Mwanamume huyo mwenye umri wa miaka 30, ambaye pia ni kasisi alitoweka baada ya kutoroka katika Hospitali ya Kaunti Ndogo ya Kapkatet alikokuwa amelazwa.
Kaka yake, Edgar, alifichua kwamba kabla ya kutoroka hospitalini, aligundulika kuwa na malaria ya ubongo, hali mbaya na inayoweza kutishia maisha.
Kipkoech alipatikana Jumanne, Juni 3, akirandaranda katika mitaa ya Litein na alirejeshwa hospitalini kwa matibabu.
Read ENGLISH VERSION
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsApp: 0732482690.
Chanzo: TUKO.co.ke