Allois Cheruiyot: Ujumbe wa Mwisho wa WhatsApp, Picha Mlimani Kabla ya kifo cha Padri Zagusa Wengi

Allois Cheruiyot: Ujumbe wa Mwisho wa WhatsApp, Picha Mlimani Kabla ya kifo cha Padri Zagusa Wengi

  • Ujumbe wa WhatsApp unaofichua jinsi Padri Allois Cheruiyot alivyotumia muda wake wa mwisho duniani umeumiza zaidi Wakatoliki na Wakenya wengine
  • Kulingana na Padri Allois, alikuwa milimani na alikuwa ametoka kuhudhuria mkutano wa jumuiya, ambao huhusisha waumini kukutana kwa ajili ya sala na mahubiri
  • Milimani, Padri alionekana mwenye furaha na ameridhika, akiwa amevaa mavazi yake ya kikuhani, akiwa na kibegi kidogo na fimbo ya kutembelea

Kaunti ya Elgeyo Marakwet: Ujumbe wa WhatsApp kutoka kwa Allois Cheruiyot ukionyesha jinsi alivyokuwa akifurahia kabla ya kifo chake umeguswa mioyo ya wengi hadi kulia.

Allois Cheruiyot: Ujumbe wa Mwisho wa WhatsApp na Picha Mlimani kabla ya kifo Zawagusa Wengi
Picha za mwisho za Allois Cheruiyot kutoka milimani. Picha: Anyama Wa Anyama.
Chanzo: Facebook

Padri Allois alikufia wapi?

Kwa masikitiko makubwa, mtumishi huyo wa Mungu alipigwa risasi hadi kufa katika Bonde la Kerio, kaunti ya Elgeyo Marakwet, na habari hizo ziliwashangaza wengi kwani hakuwa tu baba wa kiroho, bali pia alikuwa mtumishi mwaminifu wa jamii yake.

Katika picha iliyoshirikiwa na Erastus Mwenda kwenye Facebook, marehemu Padri Allois Cheruiyot anaonekana akiwa amesimama kwa kutegemea fimbo na ameketi juu ya jiwe kubwa. Alikuwa amevaa kanzu ya kikuhani ya rangi nyeusi, suruali za kijivu, na viatu vya rangi nyeusi.

Ujumbe wa Allois ulisema nini?

Pembeni yake kulikuwa na kibegi kidogo cheusi kilichoashiria kuwa alikuwa na nia ya kukaa eneo hilo kwa muda fulani.

"Otherwise, niko mlimani jumia. Jumuiya ni mkutano mdogo ambapo Wakatoliki hukutana kushiriki neno la Mungu siku za wiki, tofauti na Jumapili."

Katika picha nyingine, anaonekana akizungumza na watoto wadogo huku akiwa amevaa mavazi yale yale – mojawapo ya picha zilizoonyesha kuwa alikuwa mkarimu na aligusa maisha ya wengi, wakiwemo watoto wadogo.

Erastus Mwenda, aliyeshiriki picha yake, alisema kuwa aliumizwa sana na kifo hicho.

"Mpendwa Bonde la Kerio, tuliwapa kasisi aliyekuwa na silaha ya rozari, biblia, sakramenti, maji ya baraka na ari ya kuhudumu. Kuhudumu mbali, kuwafikia walio hatarini zaidi. Kufika kila siku kuhubiria hata nafsi moja, kuwa sauti ya tumaini," alisema Mwenda.

"Mlimrudisha bila uhai, akiwa na majeraha ya risasi na rozari yenye damu. Kwa nini?" aliongeza.

Allois Cheruiyot: Ujumbe wa Mwisho wa WhatsApp na Picha Mlimani kabla ya kifo Zawagusa Wengi
Allois Cheruiyot wakati wa hafla (kushoto), wakazi wa kijiji wakionyesha ghadhabu yao kuhusu kifo chake (kulia). Picha: Kanisa Katoliki.
Chanzo: Facebook

Ni nini kilichowaumiza Wakatoliki wakereketwa?

TUKO.co.ke ilipomfikia, Mwenda alikiri kuwa yeye ni Mkristo Katoliki wa kweli na kwamba kifo cha Padri huyo kilimuumiza sana.

"Ni uchungu mkubwa kumuua mtu ambaye hakuwa na silaha yoyote na alikuwa katika harakati za kuwatafuta kondoo waliopotea wa Bwana," alisema.

"Tuombe damu yao iliyoimwagika ilete mwisho wa uhalifu katika Elgeyo Marakwet," aliongeza.

Wakenya watoa maoni yao kuhusu tukio hilo:

Esther Esther Theuri:

"Salamu Maria, umejaa neema, Bwana yu pamoja nawe, umebarikiwa kuliko wanawake wote na amebarikiwa uzao wa tumbo lako Yesu. Mtakatifu Maria Mama wa Mungu utuombee sisi wenye dhambi sasa na saa ya kufa kwetu. Amina.🙏 Bwana wakumbuke mapadri wetu wote."

Eunice Nyambu:

"Na juu hii picha ni ya kupigwa na mtu mwenye kupiga picha ako?"

Mwas Kagu:

"Ni bahati mbaya sana kwamba Mbunge alipouawa, ndani ya siku mbili washukiwa walikamatwa, kasisi anauawa, anazikwa na hakuna hatua yoyote, siku ya mazishi yake mwingine anauawa... kuna upendeleo mara mbili? Mungu aturehemu."

Joanis Minor:

"Hii ni makosa kabisa. Huzuni kuu. Hawa ndio watu wanaookoa nafsi kwa ajili ya watu bora zaidi 😭 tunatumaini uchunguzi utafanyika haraka kama ilivyokuwa kwa yule mwingine. RIP padre."

Jane Wambua:

"Rambirambi zangu kwa familia na Kanisa Katoliki, ni uchungu sana kushuhudia watumishi wa Mungu 🙏 waliojitolea maisha yao wakifa kwa mateso, Mungu Mwenyezi achukue usukani na athibitishe kwa ulimwengu kuwa yeye ni Bwana. Amina."

Washukiwa 6 wa mauaji ya Allois wakamatwa

Katika habari nyingine, polisi wamewakamata washukiwa sita kuhusiana na mauaji ya Padri Allois.

Kulingana na msemaji wa Huduma ya Taifa ya Polisi (NPS), Muchiri Nyaga, walituma maafisa wa GSU katika Kijiji cha Kabartile muda mfupi baada ya mauaji na kuwakamata washukiwa.

Polisi pia walifafanua kuwa uchunguzi wa awali ulikuwa tayari umeondoa uwezekano wa uhalifu wa wizi wa mifugo au wizi wa kutumia silaha kama sababu kuu. Walidokeza kuwa shambulio dhidi ya Padri Bett lilikuwa limepangwa.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsApp: 0732482690.

Chanzo: TUKO.co.ke

Authors:
Francis Silva avatar

Francis Silva (Swahili translator) Francis M Silva ni Mkuu wa Kitengo cha Kiswahili. Ana tajriba ya miaka mingi katika taaluma ya uwanahabari hasa tafsiri, uhariri - Radio, TV na Dijitali. Yeye ni zao la Taasisi ya Mawasiliano-Umma ya Kenya (KIMC). Wasiliana naye kupitia: [email protected]

OSZAR »