MCA wa Kitui atiwa Mbaroni Baada ya Kuonekana kwenye CCTV Akiiba Vifaa vya Thamani ya KSh 1.9m
- Kurugenzi ya Upelelezi wa Jinai ilitangaza kukamatwa kwa MCA wa wadi ya Ikanga ya Kitui, Cyrus Musyoka Kisavi
- Kukamatwa huko kulifuatia kanda za CCTV zilizohusisha Kisavi na wizi wa vifaa vya simu vya rununu vya KSh 1.9 milioni, ambavyo vilikusudiwa mteja mmoja Mombasa
- Katika kisa tofauti, MCA wa Kajiado, Marush Stephen Rais Kisemei, alishtakiwa kwa matumizi mabaya ya bunduki, kumzuia afisa wa polisi, na kuleta fujo
MCA wa Kitui, Cyrus Musyoka Kisavi, amekumbwa na utata baada ya kunaswa kwenye CCTV akidaiwa kuiba vifaa vya simu vya thamani ya KSh 1.9 milioni.

Chanzo: Facebook
Je! MCA wa Kitui alifanikiwa vipi kupora vifaa na kutoroka navyo?
Kulingana na taarifa ambayo TUKO.co.ke iliitia mkononi, Kisavi alikamatwa na Kurugenzi ya Upelelezi wa Jinai (DCI) mnamo Jumanne, Juni 3, baada ya kutajwa kama mshukiwa wa wizi ulioripotiwa na Buscar Courier Services mnamo Februari 8, 2025.
"Kukamatwa kumefuatia kitambulisho chanya baada ya kanda ya CCTV ya eneo la tukio kuchambuliwa, ambayo ilirekodi mshukiwa akiondoka na kifurushi kilichokuwa kinatumwa kwa mteja huko Mombasa," taarifa ya DCI ilisoma kwa sehemu.
DCI iliongezea kuwa Musyoka, ambaye hakufichua utambulisho wake wa kisiasa, alionekana katika afisi ya wasafirishaji kwenye barabara ya River Road, Nairobi.
Alizuiliwa na maafisa wa usalama kutoka Buscar na kupelekwa Kituo Kikuu cha Polisi.
Alipofika huko, utambulisho wake ulithibitishwa, na alihamishiwa kwa wapelelezi kutoka Mombasa kwa uchunguzi zaidi.
Katika kesi tofauti, Marush Stephen Rais Kisemei, MCA wa wadi ya Oloosirkon kaunti ya Kajiado, alifikishwa mahakamani Alhamisi, Juni 6.
Alikabiliwa na mashtaka matatu, likiwemo matumizi mabaya ya bunduki, kumzuia afisa wa polisi, na kuleta fujo.
Mashtaka hayo yanatokana na pendekezo la ODDP ya Kajiado, ambayo iliidhinisha kushtakiwa kwake.
“MCA anadaiwa kutenda kosa hilo wakati askari polisi watatu wa Kituo cha Polisi cha Oloosirkon walipokwenda kuwakamata washukiwa waliohusika katika kesi ya shambulio na uharibifu mbaya eneo la Ngurunga, Emakoko. Mshukiwa mmoja Soipen Samuel alifanikiwa kukamatwa na kuwekwa kwenye gari la polisi, lakini wakati wa kujaribu kumkamata mshukiwa wa pili, mume alikataa huku mshukiwa wa tatu, Jackline house Joshua, akiwa ndani ya gari la polisi." maafisa wa DCI walisema
DCI iliripoti kuwa Marush, MCA wa eneo hilo, alifika na zaidi ya watu kumi wakiwa wamejihami kwa fimbo na visu.
Walimvamia afisa ambaye hakuwa na silaha anayemlinda mshukiwa aliyezuiliwa, Soipen Samuel, na kumwachilia kwa nguvu.
Akiwa na bastola mkononi, MCA aliongoza kundi hilo katika mashambulizi dhidi ya gari la polisi, na kutoa vitisho.
Maafisa wawili wenye silaha, waliokuwa ndani ya nyumba hiyo wakijaribu kukamatwa zaidi, waliingilia kati kumsaidia mwenzao na kufanikiwa kupambana na washambuliaji.
DCI Isinya alichukua jukumu la uchunguzi na kutuma faili ya kesi hiyo kwa ODPP, ambayo iliidhinisha kufunguliwa mashtaka.
MCA wa Kitui alazwa hospitalini baada ya kushambuliwa na umma
Mnamo Septemba 2024, Musyoka, ambaye pia anajulikana kama Sonko, aliponea chupuchupu kushambuliwa na washambuliaji wasiojulikana katika wilaya ya kati ya biashara ya Nairobi.
MCA alikabiliwa vikali na kupigwa vibaya na kundi la wanaume, na kumwacha akiwa amepoteza fahamu. Mamlaka zinaamini kuwa huenda tukio hilo lilikuwa la utambulisho kimakosa.

Chanzo: Facebook
Polisi wa Kamukunji walijibu eneo la tukio, na kumuokoa Musyoka kutoka kwa washambuliaji, ambao waliendelea kumshambulia hata baada ya kupoteza fahamu.
Baadaye alisafirishwa hadi Nairobi Hospital kwa matibabu.
MCA wa Garissa aliyejihami kwa visu awafurusha watu kwenye mkahawa
Kwingineko, MCA kutoka kaunti ya Garissa alisababisha tukio katika mkahawa mmoja baada ya kurekodiwa akiwafukuza watu waliokuwa wametembelea kituo hicho kwa huduma za ukarimu.
Noor Sheikh Farah, MCA wa wadi ya Jarajila, alitoa kisu na kuwafurusha wateja katika Hoteli ya Albeik muda mfupi baada ya Tamasha la Utamaduni la Garissa.
Tukio hilo lilizua hasira ya umma huku video hiyo ya kutatanisha ikisambaa katika mitandao ya kijamii
Dhoruba ilipotulia, Farah alijitokeza mbele na kuomba radhi kwa tukio hilo akisema hakukusudia kutatiza biashara katika hoteli hiyo.
Kulingana naye, alichokozwa na watu wawili waliokuwa nje ya eneo la kuegesha magari la hoteli hiyo, hali iliyomfanya kujibu kwa jeuri, na kusababisha taharuki iliyoishia kwenye mgahawa huo.
Masolo Mabonga, MKUU wa Masuala ya Sasa na Siasa, alisasisha makala haya kwa maelezo kuhusu MCA mwenye kisu aliyefurusha watu kutoka kwenye mkahawa.
Read ENGLISH VERSION
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsApp: 0732482690.
Chanzo: TUKO.co.ke