Ndindi Nyoro, Babu Owino Waongoza Orodha ya Wabunge Wachapa Kazi Katika Utafiti Mpya
- Mbunge wa Kiharu, Ndindi Nyoro, anaendelea kujitokeza kwa upekee miongoni mwa wenzake katika Bunge la 13 kwa utendakazi bora
- Utafiti uliofanywa na Kenya Track umeonyesha kuwa mbunge huyo anaongoza katika matumizi bora ya Hazina ya Maendeleo ya Maeneobunge ya Serikali Kuu (NG-CDF)
- Wabunge wengine waliotajwa miongoni mwa wanaofanya vyema ni Babu Owino wa Embakasi Mashariki, Kimani Ichung’wah wa Kikuyu, na Gathoni Wamuchomba wa Githunguri
PAY ATTENTION: Flexible Payment Plans Available! Invest in Yourself & See the Return with Our Affordable Copywriting Course!
Utafiti Mpya Wamtaja Ndindi Nyoro Kama Mbunge Anayefanya Vizuri Zaidi Katika Bunge la 13.

Chanzo: Twitter
Utafiti uliofanywa na Kenya Track umebaini kuwa Ndindi Nyoro ndiye mbunge anayefanya vizuri zaidi katika usimamizi wa fedha za Mfuko wa Maendeleo wa Maeneobunge ya Serikali Kuu (NG-CDF).
Kwa nini Ndindi Nyoro Ndiye Mbunge Bora Zaidi?
Utafiti huo uliangazia uwazi na uwajibikaji wa wabunge katika kusimamia mfuko huo. Vigezo vingine vilivyotumika ni pamoja na jinsi fedha zinavyotumika kusaidia elimu kupitia mgao wa bursari, ujenzi wa miundombinu ya shule, na vifaa vya kujifunzia; pamoja na maendeleo ya miundombinu kama barabara, maji, umeme na huduma za kijamii.
Katika vipengele hivyo vyote, Ndindi Nyoro alipata alama ya asilimia 82.4% katika eneo bunge lake la Kiharu.
Babu Owino wa Embakasi Mashariki alifuatia kwa nafasi ya pili kwa alama ya 72.2% katika uwazi na uwajibikaji wa NG-CDF.
Wabunge wengine waliotajwa kuwa na usimamizi mzuri wa fedha za NG-CDF ni:
- John Bwire (Taveta) – 70.5%
- Peter Salasya (Mumias Mashariki) – 70.1%
- Phylis Bartoo (Moiben) – 68.5%
- Joseph Munyoro (Kigumo) – 67.4%
- Machele Mohamed (Mvita) – 66.2%
- Mark Mwenje (Embakasi Magharibi) – 66.4%
- Gathoni Wamuchomba (Githunguri) – 65.1%
- Muhia Wanjiku (Kipipiri) – 66%
- Kimani Ichung’wah (Kikuyu) – 65.9%
- Mark Nyamita (Uriri) – 65.3%
- Silvanus Osoro (South Mugirango) – 64%
- Suzanne Kiamba (Makueni) – 63.7%
- Mohamed Abdikheir (Lafey) – 59.2%
Matokeo haya yalitokana na mahojiano na zaidi ya watu 5,400 wenye umri wa miaka 18 na kuendelea. Utafiti huo ulikuwa na kiwango cha kosa cha +/- 1.554% na uaminifu wa asilimia 94%. Washiriki walitoa maoni yao kupitia simu.
Je, NG-CDF Bado Ni Halali?
Wakati mjadala kuhusu uhalali wa Mfuko wa NG-CDF ukiendelea, Ndindi Nyoro ametoa wito kwa serikali kuu kuongeza fedha katika mfuko huo.
Ametaka pia misaada ya bursari zinazotolewa kupitia kaunti ziimarishwe.
Mbunge huyo, ambaye hadi hivi majuzi alikuwa mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti Bungeni, alisema serikali inapaswa kutilia mkazo elimu katika bajeti ya mwaka wa fedha 2025/26.

Chanzo: Twitter
Ameeleza kuwa kinyume na madai kwamba NG-CDF ni uwekezaji wa kibinafsi kwa wabunge, mfuko huo unasaidia sana wanafunzi wahitaji, hivyo unastahili kuongezewa fedha.
Aidha, Nyoro amemuomba Mdhibiti wa Bajeti kuwaruhusu magavana wa kaunti kuendelea kutoa bursari. Amesema jaribio lolote la kuvuruga utoaji wa misaada hiyo litaathiri familia nyingi.
Kwa mujibu wake, mjadala wa kama NG-CDF ni halali au la hauna maana yoyote kwa mwananchi wa kawaida.
Kwanini Raila Odinga Anapinga NG-CDF?
Kiongozi wa ODM, Raila Odinga, ni miongoni mwa wanaotaka mfuko huo ufutwe kabisa.
Amekuwa akiwalaumu wabunge kwa tamaa, akisema wanapigania fedha hizo huku wakikataa kupeleka fedha zaidi kwa serikali za kaunti.
Kwa mujibu wa Raila, wabunge wanapita mipaka yao kwa kushikilia fedha hizo, ilhali majukumu yao kikatiba ni uwakilishi, kutunga sheria, na usimamizi.
Read ENGLISH VERSION
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsApp: 0732482690.
Chanzo: TUKO.co.ke