Mjane wa Albert Ojwang, Nevnina, Afichua Mazungumzo ya WhatsApp ya Mumewe Akisherehekea Kuwa Baba

Mjane wa Albert Ojwang, Nevnina, Afichua Mazungumzo ya WhatsApp ya Mumewe Akisherehekea Kuwa Baba

  • Nevnina Onyango alishiriki ujumbe wa majonzi kumkumbuka marehemu mume wake, Albert Ojwang, katika Siku ya Akina Baba
  • Mjane huyo mchanga aliposti picha ya skrini ya mazungumzo yao ya WhatsApp, ikionyesha furaha ya Albert alipokuwa na familia yake
  • Alitafakari jinsi Siku ya Akina Baba ilivyopaswa kuwa siku maalum kwa Albert na mwanao, lakini sasa imejaa huzuni na majonzi

Mjane wa Albert Ojwang, Nevnina Onyango, amemuenzi mumewe marehemu kwa ujumbe wa hisia kali katika Siku ya Akina Baba.

Mjane wa Albert Ojwang, Nevnina, Afichua Mazungumzo ya WhatsApp ya Mumewe Akisherehekea Kuwa Baba
Mjane wa Albert Ojwang, Nevnina Onyango, amemuenzi katika Siku ya Akina Baba. Picha: Nevnina Neeiyanah.
Chanzo: UGC

Mama wa mtoto mmoja alichapisha picha ya mazungumzo yake ya WhatsApp na mumewe marehemu, ambaye alifariki akiwa mikononi mwa polisi.

Mjane wa Albert Ojwang amuenzi katika Siku ya Akina Baba

Katika picha hiyo ya skrini, Albert alieleza fahari yake kama mwanamume mwenye familia yake karibu naye.

"Kwa kweli, nina furaha tu kuwa na familia yangu yote karibu. Nakuona na G weekend. Nina baba, mama na nyanya. Inanifurahisha," aliandika Albert.

Nevnina alimjibu:

"Ni jambo zuri. Napenda hivi, mpenzi. Kuwa na mume wangu karibu, kuwaona wakwe zangu, na uhusiano mzuri nilionao na mamako unafanya mambo yawe bora zaidi."

"Shukrani kwa kuwa pale kwa ajili yake," Albert alijibu.

Akiambatanisha picha hiyo, Nevnina alisema Siku ya Akina Baba ilipaswa kuwa ya mumewe.

Nevnina alisema mumewe marehemu alikuwa na mipango na mtoto wao mdogo.

"Siku hii ya Akina Baba ilipaswa kuwa yako. Ulikuwa na mipango na mwanetu, mipango ya kicheko, ya upendo, ya kuwa pamoja tu. Badala yake, tumeachwa na ukimya, maswali, na dunia inayohisi si sawa. Tunakukosa zaidi ya maneno — si leo tu, bali kila siku. Upendo wako unaishi ndani yake, na nitahakikisha haumsahau baba aliyekuwa nawe, na maisha waliyokunyima. 💔 Tunakupenda baba G. #HakiKwaAlbertOjwang #FathersDayBilaWewe,” aliandika.

Mashabiki wake walimfariji kupitia sehemu ya maoni. Haya hapa baadhi ya maoni:

Eva Marie:

"Pole sana, rambirambi zangu za dhati."

Sylv Tasha:

"Pole sana dada. Mwenyezi Mungu akutie nguvu."

Wendy Nyachogo:

"Mungu akufariji na Albert apumzike kwa amani."

Hillary Akoko Sanja:

"Pole sana dada, utavuka haya. Si rahisi lakini uwe na ujasiri. Mungu yupo."

Marie Marie:

"Ingawa ni chungu sana, Mungu awe mfariji wako."

Atis Nyababa:

"Mungu akufariji mama, roho yake ipumzike kwa amani."

Milcah Kemuma:

"Pole sana...Mungu akutie nguvu."

John Ouma:

"Wamekukatisha maisha, lakini roho yako itaishi nasi milele. Ulikuwa na moyo thabiti kuleta mabadiliko."

Philemon Koyel:

"Inasikitisha 😞 lakini kuwa imara na uendelee kuwa na maombi."

Afandi Joan:

"Walikunyamazisha, lakini hata katika kimya, ukawa mwenye sauti kubwa. RIP Mtanzania mwenzetu."

Justus Manandu:

"Inasikitisha sana. Jifariji ndani ya Bwana."

Kuhusu mjane wa Albert Ojwang

Nevnina alisema mwalimu huyo aliyeuawa alikuwa na mipango mikubwa kwa familia yake.

Aliwasili Nairobi na mwanao mdogo huku Wakenya wakiendelea kuchanga michango ya kumsaidia.

Nambari yake ya simu ilisambaa mtandaoni na Wakenya wakaahidi kumsaidia.

Ojwang alikamatwa akiwa anakula chakula cha mchana na familia yake nyumbani kwao Kakoth, Homa Bay.

Mwandishi mahiri aliandika ujumbe wa kusisimua kwa baba ya Ojwang kwa niaba ya mtoto wake, na kuwaacha Wakenya wakiwa wameguswa.

Nevnina alishiriki mazungumzo yake ya mwisho na mumewe kabla ya kuuawa kinyama akiwa kizuizini.

Mjane huyo alikumbuka uchungu wakati mwanao alimuuliza kama ni kweli baba yake amekufa baada ya kusikia watu wakilia kwa uchungu wakimtaja.

Sakaja atamsaidiaje familia ya Ojwang?

Kama ilivyoripotiwa awali, gavana wa Nairobi Johnson Sakaja alimuelezea Ojwang kama rafiki wake wa karibu.

Kiongozi huyo wa kaunti alikutana na familia ya Ojwang katika City Hall, Nairobi, na akaahidi kuwasaidia na kutafuta haki.

Sakaja aliahidi kununua shamba na kujenga nyumba za kupangisha kwa familia hiyo, na pia kumwajiri mjane wa Ojwang pindi atakapomaliza masomo yake.

Kifo cha Ojwang mwenye umri wa miaka 31 kimekuwa mjadala mkubwa mtandaoni, huku Wakenya wengi wakieleza kukatishwa tamaa na jeshi la polisi ambalo linapaswa kuwalinda raia.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsApp: 0732482690.

Chanzo: TUKO.co.ke

Authors:
Shillah Mwadosho avatar

Shillah Mwadosho (Swahili editor) Shillah Mwadosho ni mwandishi wa habari wa TUKO.co.ke katika kitengo cha Kiswahili tangu 2019. Ana tajriba ya takriban miaka minne katika fani ya uandishi wa habari kwenye redio, televisheni na gazetini. Alipata ujuzi wa uanahabari katika taasisi ya Alphax mjini Eldoret. Yeye hujituliza kwa kusikiza muziki na kufurahia densi baada ya kazi. Email: [email protected]

OSZAR »